Hebrews 10:1-4

Dhabihu Ya Kristo Ni Mara Moja Tu

1 aSheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu. 2 bKama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi. 3 cLakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka, 4 dkwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

Copyright information for SwhNEN